KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI ZAANZISHA BLOGU
Bodi ya Wakurugenzi katika kikao chake namba 33 kilichofanyika Mkoani Dodoma tarehe 20/11/2019, kilifanya mabadiliko ya baadhi ya kasma za bajeti ya mafunzo ili fedha hizo ziende kusaidia uanzishwaji wa blogu za klabu za Waandishi wa Habari zilizopo mikoani.
Madhumuni ya kuanzishwa kwa blog hizi, ni kusaidia maendeleo katika mkoa husika kwa kuchapisha na kusambaza habari mbalimbali zinazoonyesha fursa zinazopatikana katika mikoa hiyo kupitia blog za klabu. Lakini pia blog hizi zitasaidia habari za vijijini kupata nafasi ya kusikika na kusomwa nchini kote.
Mpaka sasa jumla ya klabu za waandishi wa habari 13 zimefanikiwa kusajili na kufungua blogu zao na zinafanya kazi. Klabu hizo ni kama ifuatavyo
Shinyanga Press Club – www.shinyangapress.blogspot.com
Geita Press Club – www.geitapress.blogspot.com
Kigoma Press Club – www.kigomapress.blogspot.com
Central Press Club – www.centralpressclub.co.tz
Arusha Press Club – www.arushapressclub.blogspot.com
Njombe Press Club – www.njombepress.blogspot.com
Katavi Press Club – www.katavipress.blogspot.com
Manyara Press Club – www.manyarapress.blogspot.com
Tabora Press Club – www.taborapress.blogspot.com
Iringa Press Club – IPC Mkombozi TV (YouTube channel) https://www.youtube.com/channel/UCposvKsTmu7E9_NC6WbLaCg/featured?disable_polymer=1
Rukwa Press Club – www.rukwapress.blogspot.com
Pemba Press Club – www.pembapress.club/portal/
Mwanza Press Club – www.mwanzapressclub.co.tz
Klabu zilizobaki bado zinaendelea na usajili wa klabu zake na zitakapokuwa tayari taarifa yake itatolewa.