Home About Press Clubs Multimedia Contact Us Staff Mail

MWANZA PRESS CLUB YAENDESHA MDAHALO

22-Oct-21
Mwanza Press Club leo imeendesha mdahalo kuhusu Maadili ya Uandishi wa habari, Uhuru wa Kujieleza na Haki ya kupata taaarifa, mdahalo ambao ulifunguliwa rasmi na Afisa Habari kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bw. Abel Ngapemba ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh. Mhandisi Robert Gabriel.
Mdahalo huu umejumuisha waandishi wa habari kutoka Klabu za Waandishi wa Habari za mikoa ya Mwanza, Geita, Mara na Simiyu.
Pamoja na ushiriki huo kutoka Press Clubs, pia Mdahalo huu ulijumuisha wadau muhimu wa habari kutoka ofisi ya Mkuu ya Mkoa wa Mwanza ambayo iliwakilishwa na Afisa Habari wake Bw. Abel Ngapemba, kutoka TCRA alikuwepo Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Kanda ya Ziwa Bw. Francis Mihayo, kutoka ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, iliwakilishwa na Inspector Mwita Robert na Ofisi ya Mbunge wa jimbo la Nyamagana (Mh. Stanslaus Mabula) iliwakilishwa na Bi. Florah Magabe.
Pamoja na kujadili mambo mengi kuhusu Maadili ya Uandishi wa Habari, Haki ya kupata taarifa na Uhuru wa Kujieleza, wajumbe wa mdahalo huu wamekubaliana kuendelea kufanya mambo makubwa matano kama maazimio ya Mdahalo huo.
1. Kuitisha Mkutano mkubwa wa wadau na waandishi wa habari kanda ya ziwa kujadili changamoto zinazoikabili tasnia ya habari na utatuzi wake. Mkutano huu utaitishwa kwa ushirikiano wa TCRA kanda ya ziwa, UTPC na MPC.
2. Kuandaa utaratibu wa kuendelea kujengeana uwezo kwa kutumia midahalo na mafunzo kwa ushirikiano wa waandishi na wadau wa habari kwenye maeneo mtambuka ambayo yanawakutanisha wadau na waandishi wa habari mara kwa mara.
3. Kuendelea kutoa maoni ya kuboresha sheria zinazogusa tasnia ya habari nchini, mfano EPOCA, MSA na Statistics Act
4. Kuimarisha mahusiano kati ya waandishi wa habari na wadau wa habari hasa hasa taasisi za serikali kwa kutengeneza WhatsApp Group ili kuongeza wigo wa kupeana taarifa mara kwa mara.
5. Kufanya tafiti na kutoa machapisho yatakayoendelea kuongeza uelewa na kuhamisha masuala mazima ya Uhuru wa Kujieleza, Uhuru wa kutoa na kupata taarifa na maadili ya uandishi wa habari.
Mdahalo huu ni utekelezaji wa moja ya shughuli zilizomo kwenye mradi wa ushirikiano kati ya shirika la IMS (International Media Support) na UTPC.
Shughuli nyingine ni mafunzo kwa waandishi wa habari kuhusu ulinzi na usalama wa mwandishi wa habari, midahalo ya ulinzi na usalama kwa mwandishi wa habari, kuandaa kanuni za maadili ya uandishi wa habari na ufwatiliaji wa madhila kwenye tasnia ya habari.



CALL FOR CONSULTANCY
31-Jul-23
SIKU YA MAADHIMISHO YA REDIO DUNIANI 2022
15-Feb-22
WAMILIKI VYOMBO VYA HABARI WATAKIWA KUWALIPA WAANDISHI STAHIKI ZAO
14-Jan-22
UTPC YAPEWA TUZO
22-Oct-21
WAANDISHI WA HABARI WAPEWA MAFUNZO YA ULINZI NA USALAMA
22-Oct-21
SERIKALI YAANZA KUJENGA MAHUSIANO ENDELEVU NA WAANDISHI WA HABARI
22-Oct-21
MARA PRESS CLUB WAENDESHA MDAHALO
22-Oct-21
UTPC KUANDAA KANUNI ZA MAADILI YA UANDISHI WA HABARI
22-Oct-21
MWANZA PRESS CLUB YAENDESHA MDAHALO
22-Oct-21
WAFANYAKAZI WA UTPC WAJENGEWA UWEZO
22-Oct-21
MAHAKAMA KUU YA RUFAA MWANZA ITATOA MAAMUZI YA RUFAA YA SHERIA YA HUDUMA YA VYOMBO VYA HABARI (MSA) 2016 SIKU CHACHE ZIJAZO
19-Feb-21
NOTISI YA MKUTANO MKUU WA UTPC MWAKA 2020
08-Oct-20
UTPC YATOA FOMU ZA KUGOMBEA UJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI
08-Oct-20
KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI 11 ZAJIUNGA NA BIMA YA AFYA
07-Aug-20
KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI 17 ZAKAMILISHA UCHAGUZI WA VIONGOZI WAO
07-Aug-20
KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI ZAANZISHA BLOGU
07-Aug-20
TANZIA - TAARIFA ZA KIFO CHA ALIYEKUWA MFANYAKAZI WA UTPC NDUGU JACOB KAMBILI
30-Jul-20
UTPC YATOA VIFAA VYA KUJIKINGA NA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UGONJWA WA COVID19 KWA KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI TANZANIA.
02-Jun-20
MPC KUFAIDIKA NA VIFAA KINGA DHIDI CORONA TOKA EWURA
02-Jun-20
MPC YAPOKEA VIFAA VYA KUJIKINGA NA VIRUSI VYA CORONA(PPE) TOKA TAASISI YA THE DESK AND CHAIRS FOUNDATION
02-Jun-20
Maazimisho ya Siku ya Haki za Binadamu yafanyika Mwanza kwa kuwashirikisha wanahabari
11-Dec-19
Afisa Miradi wa Shirika la Maendeleo la Sweden (Sida) atembelea Klabu za Waandishi wa Habari
06-Dec-19
Wito watolewa kwa Waandishi wa Habari kujiendeleza kielimu.
06-Dec-19
Sida na UTPC wakutana kujadili Mpango Kazi na Bajeti wa mwaka 2020.
29-Nov-19
Rais wa UTPC afungua mafunzo kwa waandishi wa habari Dodoma
29-Nov-19
Bodi ya Wakurugenzi ya UTPC yapitisha Mpango Kazi na Bajeti kwa mwaka 2020
29-Nov-19
Mlezi wa MPC Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mheshimiwa John Mongella
11-Oct-19
UTPC Potrays the real picture of Unity - H.E Dr. Ali Mohamed Shein
10-Sep-19
JAMII FORUMS : Winners of Daudi Mwangosi Award 2019
06-Sep-19
UTPC in Zanzibar for the Annual Members General Meeting
05-Sep-19
UTPC ARM: Presentation of results
03-Jul-19
INVITATION FOR CONSULTANCY SERVICES FOR MID TERM REVIEW OF UTPC STRATEGIC PLAN 2016-2020
03-Jul-19
UTPC: Annual Review Meeting 2019
03-Jul-19
Crash Course: Press Clubs
03-Jul-19