Home About Press Clubs Multimedia Contact Us Staff Mail

Rais wa UTPC afungua mafunzo kwa waandishi wa habari Dodoma

29-Nov-19

Rais wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania (UTPC), Bwana Deo Nsokolo, amefungua rasmi mafunzo ya uandishi wa habari za Vijijini kwa wanachama wa Klabu za Waandishi wa habari nchini yaliyofanyika mkoani Dodoma.

Akifungua mafunzo hayo, Bwana Deo Nsokolo  amesema kwamba mafunzo wanayokwenda kupewa waandishi hawa ni sehemu ya utekelezaji wa shughuli za UTPC katika Mpango Mkakati wake 2016 - 2020, ambao unaelekea mwishoni.

Alisema kwamba UTPC inapenda kuona mafunzo haya yanafanyiwa kazi kwa waandishi wa habari kuandika habari ambazo zitachangia maendeleo ya mikoa husika  lakini pia kupata waandishi wa habari wabobezi kwenye eneo wanalopata mafunzo.

Aliongeza kwamba UTPC inapenda kuona katika mafunzo haya kila mtu anapata nafasi ya kushiriki lakini pia kuwepo na mchanganyiko wa wanachama na viongozi wa klabu na ndio maana mafunzo haya yanatolewa kwa utaratibu wa wanachama kuomba na kuchaguliwa.

Akijibu swali la Bwana Adam Malima, kuhusu nafasi ya UTPC katika kutetea ajira za waandishi wa habari na mikataba yao, Rais wa UTPC alisema kwamba suala la ajira ni tatizo kwenye tasnia ya habari, ila zipo jitihada ambazo zinafanywa na UTPC kwa kushirikiana na taasisi nyingine za kihabari ili kwa pamoja kutatua tatizo hili.

“Jambo la kufanya ni kwamba wamiliki wa vyombo vya habari wawathamini waandishi wao kwa kuwapa mikataba na kuwalipa vizuri ili kuboresha tasnia ya habari lakini pia kwa kufanya hivyo maadili ya uandishi wa habari yatazingatiwa kwa kuwa kila mwandishi atakuwa na uhakika wa ujira wake” -  Alisema Deo Nsokolo

Akizungumzia suala la maadili kwa wandishi wahabari, Bwana Deo Nsokolo aliwataka waandishi wa habari kutotumia tasnia ya habari kwa kutekeleza uovu wao.

“Msitumie tasnia ya habari kufanya uovu au kujificha nyuma ya uandishi wa habari kwa uovu wenu mkitegemea UTPC itawatetea, UTPC haitetei uandishi wa habari usiongizatia maadili na taaluma Kila mwandishi afanye kazi yake kwa kufuata maadili ya uandishi wa habari.” – Deo Nsokolo 

Pamoja na mambo mengine, Rais alisema kwamba, vyombo vya habari vimejaa hofu kubwa na waandishi wamekosa nguvu ya kuendelea kufanya kazi kwa uthubutu.

Bwana Nsokolo alizungumia huduma zinazotolewa na UTPC kwa Klabu za Waandishi wa habari,  alisema kwamba UTPC inafanya mambo mengi ukiachilia mbali mafunzo kwa waandishi wa habari. Alizitaja huduma hizo kamna vile kodi ya pango kwa Press Clubs zote, Internet, Maji na Umeme, vifaa kama vile compyuta na Kamera ambavyo vinapelekwa moja kwa moja kwenye klabu.

“Kwenye klabu zenu mnapashwa kuwa na intaneti wakati wote, lakini pia Klabu za waandishi wa habari zinapashwa kuwa ni ofisi zenye hadhi kwa kuwa UTPC inalipa kodi za ofisi hizo”

Rais alimaliza kwa kusema kwamba, mwaka 2020 ni ukomo wa ungozi kwa viongozi wa klabu hivyo UTPC na klabu zake wanategemea kufanya uchaguzi wa viongozi wake kwa mwaka huo. Aliwatia moyo washiriki hao kwamba wasisite kushika nafasi ya uongozi kwenye klabu au katika Bodi ya Wagurugenzi ya UTPC.

“Ikifika wakati wa uchaguzi hakikisheni mnachagua viongozi wazuri wa klabu zenu ili klabu zenu ziendelee kusimama” – Alisema Deo

Mafunzo mengine yaliyofanyika mkoani Dodoma katika wiki hiyo ni Mafunzo ya uandishi wa habari za Mazingira na mafunzo ya uandishi wa habari za Jinsia.



CALL FOR CONSULTANCY
31-Jul-23
SIKU YA MAADHIMISHO YA REDIO DUNIANI 2022
15-Feb-22
WAMILIKI VYOMBO VYA HABARI WATAKIWA KUWALIPA WAANDISHI STAHIKI ZAO
14-Jan-22
UTPC YAPEWA TUZO
22-Oct-21
WAANDISHI WA HABARI WAPEWA MAFUNZO YA ULINZI NA USALAMA
22-Oct-21
SERIKALI YAANZA KUJENGA MAHUSIANO ENDELEVU NA WAANDISHI WA HABARI
22-Oct-21
MARA PRESS CLUB WAENDESHA MDAHALO
22-Oct-21
UTPC KUANDAA KANUNI ZA MAADILI YA UANDISHI WA HABARI
22-Oct-21
MWANZA PRESS CLUB YAENDESHA MDAHALO
22-Oct-21
WAFANYAKAZI WA UTPC WAJENGEWA UWEZO
22-Oct-21
MAHAKAMA KUU YA RUFAA MWANZA ITATOA MAAMUZI YA RUFAA YA SHERIA YA HUDUMA YA VYOMBO VYA HABARI (MSA) 2016 SIKU CHACHE ZIJAZO
19-Feb-21
NOTISI YA MKUTANO MKUU WA UTPC MWAKA 2020
08-Oct-20
UTPC YATOA FOMU ZA KUGOMBEA UJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI
08-Oct-20
KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI 11 ZAJIUNGA NA BIMA YA AFYA
07-Aug-20
KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI 17 ZAKAMILISHA UCHAGUZI WA VIONGOZI WAO
07-Aug-20
KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI ZAANZISHA BLOGU
07-Aug-20
TANZIA - TAARIFA ZA KIFO CHA ALIYEKUWA MFANYAKAZI WA UTPC NDUGU JACOB KAMBILI
30-Jul-20
UTPC YATOA VIFAA VYA KUJIKINGA NA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UGONJWA WA COVID19 KWA KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI TANZANIA.
02-Jun-20
MPC KUFAIDIKA NA VIFAA KINGA DHIDI CORONA TOKA EWURA
02-Jun-20
MPC YAPOKEA VIFAA VYA KUJIKINGA NA VIRUSI VYA CORONA(PPE) TOKA TAASISI YA THE DESK AND CHAIRS FOUNDATION
02-Jun-20
Maazimisho ya Siku ya Haki za Binadamu yafanyika Mwanza kwa kuwashirikisha wanahabari
11-Dec-19
Afisa Miradi wa Shirika la Maendeleo la Sweden (Sida) atembelea Klabu za Waandishi wa Habari
06-Dec-19
Wito watolewa kwa Waandishi wa Habari kujiendeleza kielimu.
06-Dec-19
Sida na UTPC wakutana kujadili Mpango Kazi na Bajeti wa mwaka 2020.
29-Nov-19
Rais wa UTPC afungua mafunzo kwa waandishi wa habari Dodoma
29-Nov-19
Bodi ya Wakurugenzi ya UTPC yapitisha Mpango Kazi na Bajeti kwa mwaka 2020
29-Nov-19
Mlezi wa MPC Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mheshimiwa John Mongella
11-Oct-19
UTPC Potrays the real picture of Unity - H.E Dr. Ali Mohamed Shein
10-Sep-19
JAMII FORUMS : Winners of Daudi Mwangosi Award 2019
06-Sep-19
UTPC in Zanzibar for the Annual Members General Meeting
05-Sep-19
UTPC ARM: Presentation of results
03-Jul-19
INVITATION FOR CONSULTANCY SERVICES FOR MID TERM REVIEW OF UTPC STRATEGIC PLAN 2016-2020
03-Jul-19
UTPC: Annual Review Meeting 2019
03-Jul-19
Crash Course: Press Clubs
03-Jul-19