Home About Press Clubs Multimedia Contact Us Staff Mail

SERIKALI YAANZA KUJENGA MAHUSIANO ENDELEVU NA WAANDISHI WA HABARI

22-Oct-21
Mkurugenzi wa idara ya habari Maelezo na msemaji mkuu wa Serikali Ndg. Gerson Msigwa amesema Serikali imeanza kujenga mahusiano endelevu na waandishi wa habari na taasisi zinazomia waandishi wa habari nchini, hatua ambayo inalenga kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi.
Msigwa ameyasema hayo alipokutana na Rais wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa habari nchini UTPC Deogratius Nsokolo mjini Singida.
Msigwa amesema Serikali inatambua mchango wa waandishi wa habari na Press Club nchini katika kusimamia maadili na kusaidia maendeleo katika mikoa mbalimbali na ndio maana ameamua kuweka utaratibu wa kutoa taarifa za Serikali Kwa kukutana na waandishi katika mikoa mbalimbali.
Amesema hatua hiyo inawapa fursa waandishi kuuliza juu ya mkoa wao na Taifa.
"Nimemualika Rais wa UTPC hapa Singida ili kuonyesha azma ya serikali kuwathamini na kuwatumia wandishi wa habari katika mikoa yote kueleza masuala mbalimbali yanayotekelezwa na Serikali lakini Serikali kupata mrejesho kupitia kwao Kwa kuwa ndio wapo karibu zaidi na wananchi" alisema Msigwa.
Kwa upande wake Rais wa muungano wa klabu za waandishi wa habari Tanzania Deogratius Nsokolo alimshukuru Msemaji mkuu wa Serikali Kwa kutambua mchango wa UTPC na Press Clubs nchini pamoja na taasisi nyingine za habari nchini katika maendeleo ya nchi.
Alisema Press Clubs na UTPC zipo tayari kutoa ushirikiano wa dhati ili kuhakikisha wananchi habari ambazo zitawasaidia kupata maendeleo.
Nsokolo pia alimuomba Msemaji mkuu wa Serikali ambaye pia ni Mkurugenzi mkuu wa idara ya habari Maelezo kushughulikia changamoto zinazowakabili wanahabari nchini na hasa sheria, mikataba ya ajira na ujira, mambo ambayo ameahidi kiyashughulikia kupitia bodi ya ithibati itakayoundwa hivi karibuni.
Aidha Nsokolo amempongeza Msigwa Kwa ubunifu mbalimbali tangu ateuliwe kushika nyadhifa hizo, ubunifu ambao umefanya wananchi kupata taarifa za Serikali Kwa urahisi na waandishi kupata taarifa mbalimbali kupitia mikutano inayofanyika kila jumapili ya wiki.
Msemaji mkuu wa Serikali katika mkutano wake na waandishi wa habari pamoja na mambo mengine ametoa taarifa kuhusu maendeleo ya utoaji chanjo ya Uviko 19 na kuwataka wananchi kujitokeza kuchanja ili kujikinga na ugonjwa huo hatari.
 

 



CALL FOR CONSULTANCY
31-Jul-23
SIKU YA MAADHIMISHO YA REDIO DUNIANI 2022
15-Feb-22
WAMILIKI VYOMBO VYA HABARI WATAKIWA KUWALIPA WAANDISHI STAHIKI ZAO
14-Jan-22
UTPC YAPEWA TUZO
22-Oct-21
WAANDISHI WA HABARI WAPEWA MAFUNZO YA ULINZI NA USALAMA
22-Oct-21
SERIKALI YAANZA KUJENGA MAHUSIANO ENDELEVU NA WAANDISHI WA HABARI
22-Oct-21
MARA PRESS CLUB WAENDESHA MDAHALO
22-Oct-21
UTPC KUANDAA KANUNI ZA MAADILI YA UANDISHI WA HABARI
22-Oct-21
MWANZA PRESS CLUB YAENDESHA MDAHALO
22-Oct-21
WAFANYAKAZI WA UTPC WAJENGEWA UWEZO
22-Oct-21
MAHAKAMA KUU YA RUFAA MWANZA ITATOA MAAMUZI YA RUFAA YA SHERIA YA HUDUMA YA VYOMBO VYA HABARI (MSA) 2016 SIKU CHACHE ZIJAZO
19-Feb-21
NOTISI YA MKUTANO MKUU WA UTPC MWAKA 2020
08-Oct-20
UTPC YATOA FOMU ZA KUGOMBEA UJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI
08-Oct-20
KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI 11 ZAJIUNGA NA BIMA YA AFYA
07-Aug-20
KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI 17 ZAKAMILISHA UCHAGUZI WA VIONGOZI WAO
07-Aug-20
KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI ZAANZISHA BLOGU
07-Aug-20
TANZIA - TAARIFA ZA KIFO CHA ALIYEKUWA MFANYAKAZI WA UTPC NDUGU JACOB KAMBILI
30-Jul-20
UTPC YATOA VIFAA VYA KUJIKINGA NA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UGONJWA WA COVID19 KWA KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI TANZANIA.
02-Jun-20
MPC KUFAIDIKA NA VIFAA KINGA DHIDI CORONA TOKA EWURA
02-Jun-20
MPC YAPOKEA VIFAA VYA KUJIKINGA NA VIRUSI VYA CORONA(PPE) TOKA TAASISI YA THE DESK AND CHAIRS FOUNDATION
02-Jun-20
Maazimisho ya Siku ya Haki za Binadamu yafanyika Mwanza kwa kuwashirikisha wanahabari
11-Dec-19
Afisa Miradi wa Shirika la Maendeleo la Sweden (Sida) atembelea Klabu za Waandishi wa Habari
06-Dec-19
Wito watolewa kwa Waandishi wa Habari kujiendeleza kielimu.
06-Dec-19
Sida na UTPC wakutana kujadili Mpango Kazi na Bajeti wa mwaka 2020.
29-Nov-19
Rais wa UTPC afungua mafunzo kwa waandishi wa habari Dodoma
29-Nov-19
Bodi ya Wakurugenzi ya UTPC yapitisha Mpango Kazi na Bajeti kwa mwaka 2020
29-Nov-19
Mlezi wa MPC Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mheshimiwa John Mongella
11-Oct-19
UTPC Potrays the real picture of Unity - H.E Dr. Ali Mohamed Shein
10-Sep-19
JAMII FORUMS : Winners of Daudi Mwangosi Award 2019
06-Sep-19
UTPC in Zanzibar for the Annual Members General Meeting
05-Sep-19
UTPC ARM: Presentation of results
03-Jul-19
INVITATION FOR CONSULTANCY SERVICES FOR MID TERM REVIEW OF UTPC STRATEGIC PLAN 2016-2020
03-Jul-19
UTPC: Annual Review Meeting 2019
03-Jul-19
Crash Course: Press Clubs
03-Jul-19