Home About Press Clubs Multimedia Contact Us Staff Mail

Wito watolewa kwa Waandishi wa Habari kujiendeleza kielimu.

06-Dec-19

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) Mhandisi James Kilaba amewataka waandishi wa habari kote nchini kujiendeleza kielimu ili kukidhi matakwa ya kisheria, kwani TCRA itaendelea kuchukua hatua za kisheria kwa waandishi wote watakaokosa vigezo, lengo likiwa ni kuendelea kuimarisha tasnia ya habari nchini, lakini pia kusimamia maudhui na kuleta mshikamano na amani nchini.

Aliyasema hayo hivi karibuni katika Mkutano wa majadiliano kati ya Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) na waandishi wa Habari wa Mkoa wa Mwanza yaliyoandaliwa na Klabu Ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Mwanza (MPC).

Aliongeza kuwa TCRA itaendelea kuchukua hatua kwa lengo la kuimarisha usimamizi wa maudhui mitandaoni, ikiwa ni pamoja na kuwa na vitendea kazi vya kisasa na raslimali watu wa kutosha ili kuleta ufanisi kwenye sekta ya mawalisiano.

Pamoja na hayo, Bw. Kilaba alisema kuwa sheria ya habari ya mwaka 2016 inamtaka kila mwandishi kuwa na elimu ya kuanzia ngazi ya “Diploma” ambapo serikali imetoa kipindi cha mpito cha muda wa miaka 5 kitakachondelea hadi tarehe 31 Disemba, 2021, ili kutoa nafasi kwa kila mwandishi kujiendeleza kielimu na kufika ngazi ya Diploma.

Hata hivyo Bw. Kilaba aliwaambia waandishi hao kuwa, TCRA ilitoa kumbusho kwa wamiliki wa vyombo vya habari nchini kuzingatia matakwa ya sheria na masharti ya leseni za utangazaji kwa kuhakikisha kuwa wanaotangaza katika vyombo vyao wanakuwa na vigezo vya kitaaluma kama waandishi wa habari.

Naye Mkurugenzi wa UTPC Bw. Abubakar Karsan, alitoa wito kwa waandishi wa habari kuhakikisha wanafuata sheria wakati wanatekeleza majukumu yao ya kila siku.

Pamoja na wito huo, Bw. Karsan alitoa shukrani kwa Mkurugenzi wa TCRA kwa kukubali kushiriki kwenye mkutano huo maalumu kwa waandishi wa habari mkoa wa Mwanza.

Pia aliongeza kuwa, mwaka 2020 UTPC imeandaa mpango maalumu wa kuziwezesha klabu zote 28 nchini kusajili blog zao ili iwe rahisi kuchapisha habari nyingi za mkoa husika na kusaidia kuleta maendeleo ya Mkoa na nchi kwa ujumla. 



CALL FOR CONSULTANCY
31-Jul-23
SIKU YA MAADHIMISHO YA REDIO DUNIANI 2022
15-Feb-22
WAMILIKI VYOMBO VYA HABARI WATAKIWA KUWALIPA WAANDISHI STAHIKI ZAO
14-Jan-22
UTPC YAPEWA TUZO
22-Oct-21
WAANDISHI WA HABARI WAPEWA MAFUNZO YA ULINZI NA USALAMA
22-Oct-21
SERIKALI YAANZA KUJENGA MAHUSIANO ENDELEVU NA WAANDISHI WA HABARI
22-Oct-21
MARA PRESS CLUB WAENDESHA MDAHALO
22-Oct-21
UTPC KUANDAA KANUNI ZA MAADILI YA UANDISHI WA HABARI
22-Oct-21
MWANZA PRESS CLUB YAENDESHA MDAHALO
22-Oct-21
WAFANYAKAZI WA UTPC WAJENGEWA UWEZO
22-Oct-21
MAHAKAMA KUU YA RUFAA MWANZA ITATOA MAAMUZI YA RUFAA YA SHERIA YA HUDUMA YA VYOMBO VYA HABARI (MSA) 2016 SIKU CHACHE ZIJAZO
19-Feb-21
NOTISI YA MKUTANO MKUU WA UTPC MWAKA 2020
08-Oct-20
UTPC YATOA FOMU ZA KUGOMBEA UJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI
08-Oct-20
KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI 11 ZAJIUNGA NA BIMA YA AFYA
07-Aug-20
KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI 17 ZAKAMILISHA UCHAGUZI WA VIONGOZI WAO
07-Aug-20
KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI ZAANZISHA BLOGU
07-Aug-20
TANZIA - TAARIFA ZA KIFO CHA ALIYEKUWA MFANYAKAZI WA UTPC NDUGU JACOB KAMBILI
30-Jul-20
UTPC YATOA VIFAA VYA KUJIKINGA NA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UGONJWA WA COVID19 KWA KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI TANZANIA.
02-Jun-20
MPC KUFAIDIKA NA VIFAA KINGA DHIDI CORONA TOKA EWURA
02-Jun-20
MPC YAPOKEA VIFAA VYA KUJIKINGA NA VIRUSI VYA CORONA(PPE) TOKA TAASISI YA THE DESK AND CHAIRS FOUNDATION
02-Jun-20
Maazimisho ya Siku ya Haki za Binadamu yafanyika Mwanza kwa kuwashirikisha wanahabari
11-Dec-19
Afisa Miradi wa Shirika la Maendeleo la Sweden (Sida) atembelea Klabu za Waandishi wa Habari
06-Dec-19
Wito watolewa kwa Waandishi wa Habari kujiendeleza kielimu.
06-Dec-19
Sida na UTPC wakutana kujadili Mpango Kazi na Bajeti wa mwaka 2020.
29-Nov-19
Rais wa UTPC afungua mafunzo kwa waandishi wa habari Dodoma
29-Nov-19
Bodi ya Wakurugenzi ya UTPC yapitisha Mpango Kazi na Bajeti kwa mwaka 2020
29-Nov-19
Mlezi wa MPC Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mheshimiwa John Mongella
11-Oct-19
UTPC Potrays the real picture of Unity - H.E Dr. Ali Mohamed Shein
10-Sep-19
JAMII FORUMS : Winners of Daudi Mwangosi Award 2019
06-Sep-19
UTPC in Zanzibar for the Annual Members General Meeting
05-Sep-19
UTPC ARM: Presentation of results
03-Jul-19
INVITATION FOR CONSULTANCY SERVICES FOR MID TERM REVIEW OF UTPC STRATEGIC PLAN 2016-2020
03-Jul-19
UTPC: Annual Review Meeting 2019
03-Jul-19
Crash Course: Press Clubs
03-Jul-19