- Oct 22,2021
- General
Discover the newest articles and updates from our blog, covering a variety of engaging topics.
Leo Februari 19, 2021 Mahakama ya Rufaa Mkoani Mwanza, imesikilizwa kesi ya rufaa ambayo ilifunguliwa na UTPC na Halihalisi publishers dhidi ya sheria ya huduma za vyombo vya Habari (MSA), 2016 baada ya Mahakama kuu kutoa hukumu yake mwaka 2018.
Katika rufaa hii, UTPC na Halihalisi wamewakilishwa na mawakili Edwin Aron Hans na Jeremiah Mtobesya.
Mawakili wa UTPC na Halihalisi waliwasilisha rufaa hiyo mbele ya majaji wa Mahakama ya rufaa mkoani Mwanza na mbele ya mawakili wa serikali.
Mwaka 2017, UTPC na Halihalisi Publishers walifungua kesi ya kikatiba dhidi ya Mwanashiria Mkuu wa Serikali kupinga sheria ya Huduma ya Vyombo vya Habari ambayo inakiuka misingi ya kikatiba kuhusu Uhuru wa Kujieleza na Uhuru wa Vyombo vya Habari.
Baada ya majadiliano marefu, Majaji wa rufani wameeleza kutoa maamuzi ya rufaa hiyo baada ya siku chache kutoka leo.
Notisi hii imetolewa kwa wanachama wote wa UTPC, kwa mujibu wa kifungu namba 14 (Viii) cha katiba ya UTPC, kwamba Mkutano Mkuu wa wa UTPC kwa mwaka 2020 utafanyika tarehe 16 na 17 Novemba 2020, kwenye Ukumbi wa Flomi Hotel, Morogoro.
Ajenda zitakazojadiliwa kwenye mkutano huo ni;
KufunguaMkutano
KuthibitishaajendazaMkutano
Kupokea,kujadilinakuidhinishamuhtasariwaMkutanoMkuuwamwaka 2019
YatokanayonamuhtasariwaMkutanoMkuuwamwaka2019
Kupokea,kujadilinakupitishataarifayaUtekelezajinataarifayaukaguzi wa hesabu za UTPC kwa mwaka 2019
UchaguziwaWajumbewaBodiyaWakurugenzi
MengineyokwaidhiniyaMwenyekiti
KufungaMkutano
Imetolewa na
Mkurugenzi Mtendaji wa UTPC
Abubakar Karsan