Event

Latest from our posts

Discover the newest articles and updates from our blog, covering a variety of engaging topics.

Blog

MARA PRESS CLUB WAENDESHA MDAHALO

Mdahalo kuhusu Uhuru wa Kujieleza, Haki ya kupata taarifa na Maadili ya Uandishi wa Habari umemalizika leo mkoani Mara.
Mdahalo huu umeandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari mkoa wa Mara (MRPC) chini ya ufadhili wa IMS na UTPC.
Mdahalo huu umejadili kuhusu umuhimu wa Uhuru wa Kijieleza na Haki ya kupata taarifa namna vinavyochangia kuwa na jamii yenye taarifa na inayoweza kufanya maamuzi sahihi.
Mbali na hilo, washiriki wameazimia mambo mengine mengi ikiwemo kuendelea kutoa maoni kwa ajili ya kuboresha sheria zinazominya uhuru wa habari nchini lakini pia kuwepo kwa chombo maalumu kitakacho tetea maslahi ya waandishi wa habari Tanzania.
Read More
Blog

UTPC KUANDAA KANUNI ZA MAADILI YA UANDISHI WA HABARI

Mchakato wa kukusanya maoni kuhusu uandaaji wa kanuni za maadili ya uandishi wa habari wakiwemo watoa maudhui mtandaoni, umemalizika leo mkoani Mwanza kwa Mwanza Press Club kushiriki kama klabu ya mwisho kuandaa mkutano huu.
Tangu mchakato huu umeanza, klabu za waandishi wa habari 28 zimeshirikishwa kwenye mchakato huu kwa nyakati tofauti.
Klabu za Waandishi wa Habari ambazo zilipewa nafasi ya kuandaa mikutano hii na kutoa nafasi kwa klabu za jirani kutuma wawakilishi wao ni Dar es Salaam, Arusha, Zanzibar, Kigoma, Iringa, Dodoma, Mtwara na Mwanza.
Mikutano hii ni moja ya utekelezaji wa shughuli zilizopo kwenye mradi wa ushirikiano kati ya UTPC na IMS (International Media Support) ambao mradi huu umelenga kuzijengea uwezo taasisi za kihabari kushiriki katika ushawishi kuhusu uhuru wa habari na uhuru wa wananchi kupata taarifa.
Mradi huu unaendeshwa na shirika la International Media Support la nchini Denmark, ambao wamefadhiliwa na Umoja wa Ulaya (European Union).
Read More
Blog

MWANZA PRESS CLUB YAENDESHA MDAHALO

Mwanza Press Club leo imeendesha mdahalo kuhusu Maadili ya Uandishi wa habari, Uhuru wa Kujieleza na Haki ya kupata taaarifa, mdahalo ambao ulifunguliwa rasmi na Afisa Habari kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bw. Abel Ngapemba ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh. Mhandisi Robert Gabriel.
Mdahalo huu umejumuisha waandishi wa habari kutoka Klabu za Waandishi wa Habari za mikoa ya Mwanza, Geita, Mara na Simiyu.
Pamoja na ushiriki huo kutoka Press Clubs, pia Mdahalo huu ulijumuisha wadau muhimu wa habari kutoka ofisi ya Mkuu ya Mkoa wa Mwanza ambayo iliwakilishwa na Afisa Habari wake Bw. Abel Ngapemba, kutoka TCRA alikuwepo Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Kanda ya Ziwa Bw. Francis Mihayo, kutoka ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, iliwakilishwa na Inspector Mwita Robert na Ofisi ya Mbunge wa jimbo la Nyamagana (Mh. Stanslaus Mabula) iliwakilishwa na Bi. Florah Magabe.
Pamoja na kujadili mambo mengi kuhusu Maadili ya Uandishi wa Habari, Haki ya kupata taarifa na Uhuru wa Kujieleza, wajumbe wa mdahalo huu wamekubaliana kuendelea kufanya mambo makubwa matano kama maazimio ya Mdahalo huo.
1. Kuitisha Mkutano mkubwa wa wadau na waandishi wa habari kanda ya ziwa kujadili changamoto zinazoikabili tasnia ya habari na utatuzi wake. Mkutano huu utaitishwa kwa ushirikiano wa TCRA kanda ya ziwa, UTPC na MPC.
2. Kuandaa utaratibu wa kuendelea kujengeana uwezo kwa kutumia midahalo na mafunzo kwa ushirikiano wa waandishi na wadau wa habari kwenye maeneo mtambuka ambayo yanawakutanisha wadau na waandishi wa habari mara kwa mara.
3. Kuendelea kutoa maoni ya kuboresha sheria zinazogusa tasnia ya habari nchini, mfano EPOCA, MSA na Statistics Act
4. Kuimarisha mahusiano kati ya waandishi wa habari na wadau wa habari hasa hasa taasisi za serikali kwa kutengeneza WhatsApp Group ili kuongeza wigo wa kupeana taarifa mara kwa mara.
5. Kufanya tafiti na kutoa machapisho yatakayoendelea kuongeza uelewa na kuhamisha masuala mazima ya Uhuru wa Kujieleza, Uhuru wa kutoa na kupata taarifa na maadili ya uandishi wa habari.
Mdahalo huu ni utekelezaji wa moja ya shughuli zilizomo kwenye mradi wa ushirikiano kati ya shirika la IMS (International Media Support) na UTPC.
Shughuli nyingine ni mafunzo kwa waandishi wa habari kuhusu ulinzi na usalama wa mwandishi wa habari, midahalo ya ulinzi na usalama kwa mwandishi wa habari, kuandaa kanuni za maadili ya uandishi wa habari na ufwatiliaji wa madhila kwenye tasnia ya habari.
Read More
Blog

WAFANYAKAZI WA UTPC WAJENGEWA UWEZO

Mafunzo ya ndani ya siku tatu kwa wafanyakazi wa UTPC ya namna bora ya kufanya Tathmini na Ufuatiliaji wa miradi (Monitoring and Evaluation) yamemalizika katika ofisi za UTPC.
Mafunzo haya yamewezeshwa na shirika la IMS ambalo UTPC inafanya nalo kazi kupitia mradi wa ushirikiano unaolenga kuzingea uwezo taasisi za kihabari nchini kushiriki kwenye ushawishi wa kuboresha uhuru wa habari, uhuru wa wananchi kupata taarifa na upatikanaji wa haki za msingi.
Mashirika mengine yanayotekeleza mradi huu na ambayo yamejengewa uwezo ni MISA TAN, TAMWA, MULIKA na ZANZIBAR YOUTH FORUM
Read More
Blog

MAHAKAMA KUU YA RUFAA MWANZA ITATOA MAAMUZI YA RUFAA YA SHERIA YA HUDUMA YA VYOMBO VYA HABARI (MSA) 2016 SIKU CHACHE ZIJAZO

Leo Februari 19, 2021  Mahakama ya Rufaa Mkoani Mwanza, imesikilizwa  kesi ya rufaa ambayo ilifunguliwa na UTPC na Halihalisi publishers dhidi ya sheria ya huduma za vyombo vya Habari (MSA), 2016 baada ya Mahakama kuu kutoa hukumu yake mwaka 2018.

 

Katika rufaa hii, UTPC na Halihalisi wamewakilishwa na mawakili Edwin Aron Hans na Jeremiah Mtobesya.

Mawakili wa UTPC na Halihalisi waliwasilisha rufaa hiyo mbele ya majaji wa Mahakama ya rufaa mkoani Mwanza na mbele ya mawakili wa serikali.

 

Mwaka 2017, UTPC na Halihalisi Publishers walifungua kesi ya kikatiba dhidi ya Mwanashiria Mkuu wa Serikali kupinga sheria ya Huduma ya Vyombo vya Habari ambayo inakiuka misingi ya kikatiba kuhusu Uhuru wa Kujieleza na Uhuru wa Vyombo vya Habari.

 

Baada ya majadiliano marefu, Majaji wa rufani wameeleza kutoa maamuzi ya rufaa hiyo baada ya siku chache kutoka leo.

Read More
Blog

NOTISI YA MKUTANO MKUU WA UTPC MWAKA 2020

Notisi hii imetolewa kwa wanachama wote wa UTPC, kwa mujibu wa kifungu namba 14 (Viii) cha katiba ya UTPC, kwamba Mkutano Mkuu wa wa UTPC kwa mwaka 2020 utafanyika tarehe 16 na 17 Novemba 2020, kwenye Ukumbi wa Flomi Hotel, Morogoro.

 

Ajenda zitakazojadiliwa kwenye mkutano huo ni;

  1. KufunguaMkutano

  2. KuthibitishaajendazaMkutano

  3. Kupokea,kujadilinakuidhinishamuhtasariwaMkutanoMkuuwamwaka 2019

  4. YatokanayonamuhtasariwaMkutanoMkuuwamwaka2019

  5. Kupokea,kujadilinakupitishataarifayaUtekelezajinataarifayaukaguzi wa hesabu za UTPC kwa mwaka 2019

  6. UchaguziwaWajumbewaBodiyaWakurugenzi

  7. MengineyokwaidhiniyaMwenyekiti

  8. KufungaMkutano

     

     

     

     

Imetolewa na 

Mkurugenzi Mtendaji wa UTPC

Abubakar Karsan

Read More